mujibu wa Idara ya tarjama ya Shirika la Habari la Hawza, Sheikh Muhammad Jawad Hafizi, mwanazuoni wa Pakistani, katika khutba za Swala ya Ijumaa katika Msikiti Mkuu wa mji wa Skardu, Baltistan, Pakistan, alisisitiza umuhimu wa kulinda umoja wa Umma wa Kiislamu na kusema: Waislamu wanapaswa, kwa kuwa na tahadhari na uelewa mpana, kujiepusha na kuchochea tofauti na mifarakano, na wasiruhusu maadui kutumia mgawanyiko huo kufikia malengo yao.
Akieleza wasiwasi wake kuhusu mazingira yaliyoundwa dhidi ya Uislamu na Waislamu, aliongeza: Katika hali ya sasa, kuna umuhimu mkubwa zaidi kuliko wakati mwingine wowote kwa Umma wa Kiislamu kuzuia tofauti na nyufa za ndani, na kutoruhusu tofauti hizo kutumiwa kwa ajili ya maslahi na malengo ya makundi ya nje.
Mwanazuoni huyo wa Pakistani, huku akilaani ugaidi na misimamo mikali ya kufurutu mipaka, pamoja na juhudi za kuwafanya Waislamu wapigane wao kwa wao, alisisitiza: Umma wa Kiislamu haupaswi kukabiliana na matukio na mabadiliko kwa kuongozwa na hisia pekee; bali unapaswa, kwa kufanya uchunguzi, kuwa na uelewa, umoja na busara, kuchunguza ukweli wa mambo na kufanya maamuzi kuhusu masuala mbalimbali.
Sheikh Hafizi, akirejelea kisa cha Bani Israil katika Qur’ani Tukufu, alieleza: Mwanadamu, hata akijitahidi kwa kiasi gani kuficha ukweli na kufunika uhalisia wa mambo, hatimaye matakwa ya Mwenyezi Mungu yatakuwa ni ukweli kufichuka, na uhalisia wa mambo utadhihirika.
Maoni yako